Shambulio laua watu zaidi ya 70 Ufaransa
Shambulio laua watu zaidi ya 70 Ufaransa

Shambulio laua watu zaidi ya 70 Ufaransa

Zaidi ya watu 70 wameripotiwa kuuawa katika shambulio lililotokea katika mji wa Nice kaskazini mwa Ufaransa.

Lori lililokuwa likienda mwendo kasi lilijiingiza katika mkusanyiko wa watu waliokuwa wakiangalia maonesho ya fataki kuadhimisha siku ya kitaifa ya Bastille, ambayo huja na shamra shamra kila mwaka.

Mwendesha mashtaka katika mji wa Nice, Jean- Michel Pretre amesema lori hilo liliendelea kutembea kilo mita mbili kabla ya polisi kumpiga risasi dereva.

Bunduki na makombora yameripotiwa kukutwa ndani ya lori hilo.

Waakazi wa mji huo wa Nice wameshauriwa kutulia majumbani.

Atentado Niza: Al menos 80 muertos y 16 heridos en estado crítico al arrollar un camión a la multitud en Niza

Rais Francois Hollande amerudi mjini Paris kwa ajili ya kufanya kikao cha dharura.

Forças de Segurança

Hali ya tahadhari iliyowekwa toka kutokea kwa shambulio lililofanywa na Islamic State mjini Paris, bado iko palepale nchini Ufaransa.

PERCEPTIONS

Related posts